Home » » Mbunge wa CCM ailipua serikali matokeo mabaya kidato cha nne

Mbunge wa CCM ailipua serikali matokeo mabaya kidato cha nne

Mbunge wa Ngara (CCM), Deogratias Ntukamazina
Kasi ya wabunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kukosoa utekelezaji wa serikali ya Rais Jakaya Kikwete inazidi kuongezeka ndani ya Bunge.

Jana, Mbunge wa Ngara (CCM), Deogratias Ntukamazina, aliikosoa serikali hiyo kwa kuyafuta matokeo ya mtihani wa kidato cha nne kwa mwaka 2012, kisha kuyatangaza utangaza upya hivi karibuni.

Ntukamazina ambaye kitaaluma ni Mwalimu, alisema hatua hiyo ni ya kisiasa zaidi na mfano wa ‘danganya toto’ inayofanywa na serikali kwa umma.

Ntukamazina alisema hayo wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa mwaka 2013/2014, iliyowasilishwa na waziri wake, Dk Shukuru Kawambwa.

Alisema matokeo yanapofutwa, kinachofuata ni kufanyika upya na si kuyapitia (matokeo hayo)  kisiasa na kuyatangaza kwa wananchi.

Mbunge huyo alisema haifai kwa serikali kufanya siasa kwa mambo ya msingi kama elimu, na kukumbusha kuwa hata mtawala wa mwisho wa kikoloni kuondoka nchini alitahadhalisha hivyo.

Alisema, mtawala huyo, Gavana  Richard Turnbull, (wakati akiondoka) alimwambia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, kuwa anaweza kufanya siasa kwa mambo yote ya kijamii isipokuwa elimu.

Ntukamazina alielezea kushangazwa na hatua iliyofikiwa na Dk Kawambwa, kutangaza matokeo hayo kinyume cha taratibu. Alisema mamlaka yenye kutangaza matokeo hayo yapo kwa Baraza la Mitihani

Hata hivyo, Ntukamazina alisema jamii ina wajibu wa kushiriki kurekebisha mfumo wa elimu na kuinua kiwango cha ufaulu, kupitia malezi bora na kuwaepusha watoto dhidi ya tamaduni za kimagharibi.

“Nimekuwa Mwalimu tangu mwaka 1973, sijawahi kumuona Waziri akitangaza mitihani, hiyo ni kazi ya Baraza la Mitihani… msiingie jikoni, mtaungua,” alionya.

Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Naomi Kaihura, alisema kinachokwamisha ufanisi katika mambo ya msingi ya jamii kama elimu, ni kwa baadhi ya wabunge kuwa ‘vigeugeu’.

Alisema wabunge wanapokuwa kwenye Kamati za Bunge ama nje ya ukumbi huo, wanaongea mambo ya msingi yenye maslahi, lakini wanapoingia bungeni wanachangia tofauti, huku wakiwalinda waovu na uovu.

Nimefundisha 40 yrs.  Miporomoko na mianguko ya elimu nimeiona na kuishuhudia. Nchi ni wamoja, tukimbie mapepo, mahali hapo tutaongea lugha inayoeleweka.

Mbunge wa Mchinga (CCM), Said Mtanda, alishutumu mgawanyo usio sawa wa ukarabati wa shule na kusema imeupendelea zaidi mkoa wa Kilimanjaro.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive

Popular Posts

.

CHAT BOX

My Blog List

 
Support : BONGOCLANTZ
Copyright © 2013. KANGAROO - All Rights Reserved
Template Created by EDDIE SUCRE
Proudly powered by Blogger