Home » » Mambo motomoto Fainali tuzo za Kili

Mambo motomoto Fainali tuzo za Kili


KITUO cha runinga cha ITV kitaonesha moja kwa moja fainali za tuzo ya muziki za Kilimanjaro zinazotarajiwa kufanyika Juni 8 kwenye ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alisema, sababu za kuichagua ITV ni kuamini wanaweza kufanya kazi hiyo kwa ufanisi.
Pamoja na fainali hizo kuoneshwa moja kwa moja ITV, Kavishe alisema pia litaoneshwa sehemu tatu tofauti kwenye maeneo ya wazi. Alizitaja sehemu hizo kuwa ni Mwanza eneo la Mabatini, Temeke Uwanja wa Taifa na Kilimanjaro CCM Mkoa.
Kavishe alisema zoezi la kupigia kura wasanii kuelekea tuzo hizo zinazokwenda na kaulimbiu ya Kikwetukwetu mwaka huu lilifungwa Mei 31.
Kuhusu burudani katika usiku huo, Kavishe alisema kwamba wasanii wa sasa wataimba nyimbo za wasanii wa zamani na wasanii wa zamani wataimba nyimbo za wasanii wa sasa.

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive

Popular Posts

.

CHAT BOX

My Blog List

 
Support : BONGOCLANTZ
Copyright © 2013. KANGAROO - All Rights Reserved
Template Created by EDDIE SUCRE
Proudly powered by Blogger