Nyota wa muziki wa hip hop, Joh Makini |
Tamasha hilo lilikuwa maalum kwa ajili wa uzinduzi wa kinywaji kipya cha Coca-cola Zero kinachotolewa na kampuni ya kutengeneza na kusambaza vinywaji baridi jamii ya Coca-Cola ya Bonite Bottlers yenye makao yake mjini Moshi.
Burudani hiyo ya aina yake ilianza saa nane mchana kwa vijana waendesha pikipiki kuonyesha umahiri wao wa kutawala chombo hicho cha moto kabla ya wasanii wanaoinukia wa hip hop, Paul Mushi na Juma Abdallah, kupanda stejini na kupokewa kwa shangwe na maelfu ya wapenzi wa muziki waliojitokeza kushuhudia tamasha hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari katika tukio hilo, Mkurungenzi Mkuu wa Mauzo wa kampuni ya Bonite Bottlers, Christopher Loiruk, alisema kampuni yake imeandaa tamasha hilo kwa ajili ya kuitambulisha Coke Zero na pia kuburudika pamoja na wateja wake.
"Bonite Bottlers tumekuwa mstari wa mbele katika kudhamini michezo na kuendeleza vipaji vya vijana, na leo tumeona kikundi kipya kabisa cha muziki wa hiphop kikipata nafasi ya kuonyesha umahiri. Wapenzi wa muziki watakubaliana nami kwamba kama vijana hawa wataendelea kupewa fursa na kuwezeshwa watakuwa wasanii wakubwa sana nchini," alisema Loiruk.
Naye Meneja Bidhaa ya Coca-Cola Tanzania, Maurice Njolowa alisema nia ya kampuni yake ni kuweka kinywaji kipya cha kampuni hiyo cha Coke Zero karibu na vijana na kwamba kuandaa tamasha la bure kama hilo ndiyo njia nzuri ya kuwa karibu nao.
Tamasha hilo ni muendelezo wa matamasha ya Coke Zero yaliyoanzia Coco Beach jijini Dar es Salaam wakati kinywaji hicho kisicho na sukari kilipozinduliwa Machi mwaka huu. Tamasha jingine la Coke Zero litafanyika jijini Mwanza hivi karibuni.
0 comments:
Post a Comment