Home » » Stars, Morocco kuumana saa 5 usiku

Stars, Morocco kuumana saa 5 usiku

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah
Mechi ya marudiano ya ya Kundi C la kuwania kufuzu kushiriki fainali zijazo za Kombe la Dunia kati ya timu ya taifa ya Morocco (Simba wa Atlas) na timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itachezwa Jumamosi usiku jijini Marrakech, Morocco, imeelezwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah alisema kuwa mechi hiyo itachezwa kuanzia saa 3:00 usiku kwa saa za jiji la Marrakech muda ambao itakuwa saa tano usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Osiah huyo alisema kuwa kikosi cha wachezaji 21 cha Taifa Stars jana kiliwasili salama jijini Marrakech kikitokea Ethiopia ambako kilicheza mechi ya kimataifa ya kirafiki inayotambuliowa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) dhidi ya timu ya timu ya taifa ya Sudan kwenye Uwanja wa Addis Ababa Jumapili. Timu hizo zilitoka suluhu.

Alisema kuwa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imefikia hoteli ya Pullman ambayo pia ilikaa timu ya taifa ya Ivory Coast ilipokwenda kucheza dhidi ya Morocco na kwamba washambuliaji wawili wa Stars, Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu walitarajiwa kuwasili jana saa 8 mchana wakitokea Maputo, Msumbiji ambapo timu yao ya TP Mazembe ilikuwa na mechi ya Kombe la Shirikisho.

"Timu itarejea nchini Juni 9 (Jumapili) kujiandaa kwa mechi nyingine ya marudiano ya Kundi C dhidi Ivory Coast itakayochezwa nchini (Tanzania) wiki moja baadaye (Juni 16)," alisema Osiah.

Katika mechi ya awali iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Machi 24 mwaka huu, Stars iliibuka na ushindi wa 3-1. Shukrani kwa magoli ya Samatta, aliyefunga magoli mawili na Ulimwengu.

Mabingwa wa Afrika wa mwaka 1992, Ivory Coast, wanaongoza msimamo wa kundi hilo wakiwa na pointi 7, moja nyuma ya Tanzania wanaokamata nafasi ya pili wakifuatwa na mabingwa wa Afrika mwaka 1976, Morocco, wenye pointi mbili huku Gambia wakishika mkia baada ya kuambulia pointi moja tu baada ya kila timu kucheza mechi tatu.
 

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive

Popular Posts

.

CHAT BOX

My Blog List

 
Support : BONGOCLANTZ
Copyright © 2013. KANGAROO - All Rights Reserved
Template Created by EDDIE SUCRE
Proudly powered by Blogger