Home » » Makinda ashiriki ibada ya kumwombea Mwalimu Nyerere

Makinda ashiriki ibada ya kumwombea Mwalimu Nyerere

Spika wa Bunge, Anne Makinda
Spika wa Bunge, Anne Makinda, ameshiriki ibada ya maombi maalum kwa ajili ya kumuombea Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julisu Nyerere.

Maombi hayo yalifanyika katika mji wa Namgongo nchini Uganda yakiwa na lengo la kumtangaza Mwalimu Nyerere kuwa mwenye heri na hatimaye mtakatifu kulingana na na imani ya dhehebu la kikatoliki.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari, maombi hayo maalum hufanyika Juni Mosi kila mwaka kwa mfululizo wa siku saba.

Makamu wa Rais wa Uganda, Edward Ssekandi, ambaye alimwakilisha  Rais Yoweri Kaguta Mseven alisema mwalimu Nyerere katika maisha yake alikuwa mtetezi wa haki za wanyonge na kupigania uhuru wa Mwafrika.

Alisema Mwalimu Nyerere alijipatia sifa ndani na  nje ya nchi yake na  kwamba kamwe wananchi wa Uganda hawawezi kumsahau kwa ajili ya vita vya ukombozi wa nchi yao vya mwaka 1978 hadi 1979.

Viongozi wengine walioshiriki  ibada hiyo ni Waziri Mkuu Mstaafu, John Samwel Malecela, Mama Maria Nyerere na watoto wake watatu, akiwamo Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki,  Charles Makongoro Nyerere.

0 comments:

Post a Comment

Blog Archive

Popular Posts

.

CHAT BOX

My Blog List

 
Support : BONGOCLANTZ
Copyright © 2013. KANGAROO - All Rights Reserved
Template Created by EDDIE SUCRE
Proudly powered by Blogger