OPARESHENI
Fichua Maovu 'OFM' inayoendeshwa na Magazeti ya Global Publishers
inaendelea, hivi karibuni mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la
Ezekiel Malika 'Baba Kulwa' amenaswa gesti na mkewe akiserebuka na shoga
aitwaye Aunt Steve na kuibua mtiti mzito, Ijumaa Wikienda
limekukusanyia. Tukio hilo lililovuta umati lilijiri Mei 20, mwaka huu
kwenye gesti moja (jina tunalo) iliyopo Mwananyamala, Dar ambapo mke wa
Ezekiel alivamia na kutembeza mkong’oto wa hasira kwa mumewe.
ILIKUWAJE?
Mei 19, mwaka huu, saa 3:15 asubuhi, mwanamke mmoja
ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa ajili ya heshima yake mtaani
alilipigia simu gazeti hili na kutoa malalamiko kwamba mumewe amekuwa na
tabia ya kulala na wanaume wenzake ambao ni mashoga.
“Jamani, mimi
naitwa… (akataja jina), naomba jina langu lisiandikwe gezetini.
Malalamiko yangu ni kwamba, mume wangu amekuwa na tabia ya kulala na
mashoga, hivi ninavyoongea ana ahadi ya kukutana na mmoja wao gesti kama
si kesho basi keshokutwa, niliona meseji kwenye simu ya mume wangu.
“Nawaomba
chondechonde, mnisaidie ili hii tabia ikome. Nipo tayari kusikia
maelekezo yenu kwa sababu nimesoma kwenye gazeti lenu kwamba mnafichua
maovu na huu nao ni uovu,” alisema kwa masikitiko mwanamke huyo.
MKE APEWA MAELEKEZO
Mratibu wa Oparesheni Fichua Maovu alimpa
maelekezo mwanamke huyo akimtaka kufuatilia kwenye simu ya mumewe ili
kubaini siku ya wawili hao kukutana gesti.
“Nawaahidi kwamba leo
hiihii kabla giza halijaingia nitakuwa nimejua siku yao ya kukutana,
naomba msiache kupokea simu yangu jamani.”
OFM: Sawa mama, pole sana.
Mwanamke: Asante sana.
SIMU YASUBIRIWA
Saa 11:00 jioni, mwanamke huyo alipiga simu tena kwa OFM na kupokelewa na yuleyule mratibu wake aliyempa maelekezo.
Mwanamke: Mchana wakati mume wangu amekwenda kuoga niliipekua simu yake, wanakutana kesho kwenye gesti ya …(anaitaja jina).
“Kwa hiyo mtanisaidiaje?”
OFM:
Wewe kuwa beneti na mumeo, kesho akiondoka na wewe ondoka hata kwa
kujificha, mfuatilie hadi kwenye hiyo gesti huku ukitupa mawasiliano.
Mwanamke: Hilo halina shida, nitakodi Bajaj halafu nitawaambia.
OFM: Oke, kuwa makini, mawasiliano ni muhimu. Tutawanasa kisha wakaishie polisi.
Mwanamke:
Nitashukuru sana jamani. Loo! Kweli dunia imekwisha, mwanaume ana mke,
hatosheki anatafuta wanaume wenzake, afadhali angekwenda kwa
machangudoa.”
MKE ACHUKUA MASHOSTI, WATINGA GESTI
Siku ya tukio saa 8:00 mchana,
mwanamke huyo akiwa ameongozana na mashoga zake, walifika kwenye gesti
hiyo na kubana sehemu ambayo wangeweza kumwona anayeingia na kutoka
kisha akawasiliana na mratibu wa OFM ambaye aliwatuma mapaparazi watatu
wenye kamera za kupiga picha kwa umbali wa mita 100.
Kufumba na
kufumbua, Aunt Steve aliwasili na kuzama ndani ya gesti hiyo kwa kutumia
mlango wa nyuma ili asionekane kwa vile sheria ya serikali kuhusu
gesti, wanaume hawaruhusiwi kuingia kwenye chumba kimoja.
Mapaparazi wetu wakiwa tayaritayari walitega katika pembe tatu za gesti hiyo ili kunasa tukio hilo hatua kwa hatua.
BABA KULWA NAYE HUYO
Kufumba na kufumbua, Baba Kulwa alitokea na
kuingia ndani ya gesti hiyo kwa kutumia mlango mkubwa wa mbele huku
akiwa hajui kama arobaini yake ilikuwa imebakiza dakika chache siku
hiyo.
Alifika mapokezi na kupewa chumba No. 01, akaenda uani na
kufanya jitihada kubwa za kumpitisha shoga huyo kwa mlango wa nyuma hadi
ndani.
WAACHWA KWA DAKIKA KUMI ILI…
Baada ya wote kuzama chumbani, mke wa
mwanaume huyo, mashosti zake na mapaparazi waliwaacha kwa dakika kumi
ili wafikie hatua ya kuchojoa nguo hivyo kuweza kuwanasa wakiwa
watupu...
0 comments:
Post a Comment